1. Kwa nini Umoja wa madhehebu ya kikristo Arusha hauna maono ya kununua vyombo vya mziki? kwa hakika kama kila mchungaji(kanisa) angechangia angalau 500,000 kwa mwaka naamini vingepatikana vyombo bora sana vya mziki. Kwa miaka nenda rudi changamoto ya vyombo vya mziki (PA) imekuwa sugu. wengi wa waamini ambao hawapo karibu na jukwaa kuu huwa hawapati mawasiliano vyema. Baba zetu hebu liangalieni hili.
2. Jukwaa. Kwa hali ya uwanja wowote wa mpira jukwaa kuu huwa halileti picha ya muunganiko kwa wasikilizaji. Ni vema jukwaa kuu likawekwa angalau katikati ya uwanja. Kwa nguvu ya umoja huu mkitushirikisha waamini wenu jamani hatushindwi kuchonga jukwaa bora na kubwa litakalohudumia ibada hii kwa namna ya kipekee.
3. Nyakati za nyuma tulizoea kuwa na mikutano ya injili inayohudumiwa na umoja wa madhehebu ya kikristo Arusha. Tafadhali fufueni enzi hizo ambako mikutano haikuwa kwa ajili ya kukua kwa dhehebu fulani bali kuuleta pamoja mwili wa kristo.
Je? wewe mmwenzangu una maoni gani ili umoja huu uzidi kusonga mbele?
Karibu utoe maoni yako na wewe!
No comments:
Post a Comment